-DIVISHENI ZIRO YAFUTWA
- VIWANGO VYA UFAULU VYASHUSHWA
Wanafunzi wa Kidato cha nne wakiwa wameanza mtihani siku ya leo ya tarehe 4 Novemba, 2013, Serikali imepunguza alama za ufaulu kwa mtihani huo pamoja na ule wa Kidato cha Sita.
Pia imetangaza kuwa, mitihani ya taifa wa vidato hivi tajwa hapo juu utakuwa na alama 60 za ufaulu, huku alama 40 zilizobaki zitatokana na zile za maendeleo ya mwanafunzi shuleni zinazojulikana kama CA.